Unachoweza kufanya

Elewa ponografia ni nini hasa. Ponografia ni kushushia heshima kitu ambacho Mungu aliumba kiheshimike. Kuelewa hilo kuhusu ponografia kutakusaidia ‘uchukie yaliyo mabaya.’—Zaburi 97:10.

Fikiria madhara. Ponografia huwashushia heshima wahusika. Pia inamdhalilisha mwenye kuitazama. Biblia inasema hivi kwa sababu nzuri: “Mtu mwerevu ni yule ambaye ameona msiba na kujificha.”—Methali 22:3.

Azimia. Mwanamume mwaminifu aliyeitwa Ayubu alisema hivi: “Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.” (Ayubu 31:1, Neno—Biblia Takatifu) Wewe pia unaweza ‘kufanya maagano’ yafuatayo:

Sitatumia Intaneti nikiwa peke yangu.
Nitafunga tovuti yoyote inayotokea ghafula na kuonyesha mambo machafu.
Nitazungumza na rafiki mkomavu endapo nitatumbukia tena katika tatizo hili.

Mwombe Mungu akusaidie. Mtunga-zaburi alimsihi Yehova Mungu hivi: “Geuza macho yangu kutoka kwenye mambo yasiyofaa.” (Zaburi 119:37, Neno—Biblia Takatifu) Mungu anataka ufaulu, na ukimwomba akusaidie, anaweza kukupa nguvu za kufanya yaliyo mema!—Wafilipi 4:13.

Kadiri unavyozidi kutazama ponografia ndivyo inavyokuwa vigumu kuiepuka
Zungumza na mtu. Kuchagua mtu unayeweza kumweleza mambo ya siri ni hatua muhimu inayoweza kukusaidia kuvunja mazoea hayo.—Methali 17:17.

Kumbuka hili: Kila wakati unapoepuka ponografia, unakuwa umepiga hatua kubwa sana. Mwambie Yehova Mungu kuhusu ushindi huo, na umshukuru kwa nguvu alizokupa. Unapoepuka ponografia, unafanya moyo wake ushangilie!—Methali 27:11.